

Lugha Nyingine
Umoja wa Mataifa?wasema mapigano nchini Sudan yanavuruga utaratibu wa biashara
Ofisi ya Umoja wa Mataifa Inayoratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) imesema, athari za kuvuka mpaka za mapigano yanayoendelea nchini Sudan zimeathiri sana biashara kati ya nchi hiyo na Sudan Kusini, na pia kuongeza idadi ya raia wa Sudan Kusini wanaorejea nchini humo kutoka Sudan.
OCHA imesema mapigano hayo kati ya Jeshi la Sudan na Kikosi cha Mwitikio wa Haraka (RSF) yaliyoanza katikati ya Mwezi April mwaka huu, yamepunguza uagizaji wa bidhaa kutoka nje, na hivyo kusababisha kupanda kwa bei za vyakula nchini Sudan Kusini.
Pia Ofisi hiyo imeripoti kuwa, watu 317,993 wameingia nchini Sudan Kusini kutoka Sudan tangu kuanza kwa mapigano hayo, na kuongeza kuwa, nusu ya watu hao ni wanawake, na nusu ya watoto ni wenye umri wa chini ya miaka 18.
Kutalii Hifadhi ya Taifa ya Nairobi nchini Kenya kupitia lenzi ya kamera
Habari Picha: Watu wakitembelea Mlima Huashan katika Mkoa Shaanxi, Kaskazini Magharibi mwa China
Mandhari ya Ziwa Kanas katika Eneo la Altay, Mkoa wa Xinjiang, China wakati wa majira ya mpukutiko
Katika Picha: Mandhari ya magenge kwenye Mto Manjano huko Henan, China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma