<form id="9przj"></form>

      <form id="9przj"><th id="9przj"><th id="9przj"></th></th></form>

      <form id="9przj"></form>

      <noframes id="9przj"><form id="9przj"></form>

      Mwanadiplomasia mwandamizi wa China atoa wito wa kuzuia mapigano kati ya Palestina na Israel yasizidi kuongezeka

      (CRI Online) Oktoba 24, 2023

      Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi amesema ni muhimu kuzuia hali ya kuchochea na kusababisha matatizo makubwa zaidi ya kibinadamu katika mapigano yanayoendelea kati ya Palestina na Israel.

      Waziri Wang ameyasema hayo siku ya Jumatatu alipoongea kwa simu na mwenzake wa Israel Eli Cohen, ambapo Cohen ameeleza msimamo wa Israel na wasiwasi wake wa kiusalama kuhusu mgogoro kati ya Palestina na Israel.

      Bw. Wang amebainisha kuwa China ina wasiwasi mkubwa juu ya kuendelea kwa hali ya kuchochea vita na athari zinazozidi kuwa mbaya, na kusikitishwa sana na idadi kubwa ya vifo vya raia vilivyosababishwa na vita.

      Amesema China inalaani vitendo vyote vinavyodhuru raia na kupinga ukiukaji wowote wa sheria ya kimataifa, na kuongeza kuwa nchi zote zina haki ya kujilinda, lakini zinapaswa kuheshimu sheria ya kimataifa ya kibinadamu na kulinda usalama wa raia. Hivyo amesema maafikiano ya jumuiya ya kimataifa ni kuwepo kwa suluhu ya nchi mbili.

      Wakati huohuo Bw. Wang amefanya mawasiliano kwa njia ya simu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Palestina Riyad Al–Maliki ambapo amefafanua kuwa kinachohitajika zaidi katika Ukanda wa Gaza ni juhudi za kuleta amani, usalama, chakula na dawa, badala ya vita, silaha na risasi ama hesabu za siasa za kijiografia.

      (Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

      Picha

      亚洲乱亚洲乱妇24p-JK白丝极品被CAO到流水呻吟-国产精品日韩欧美一区二区三区-欧美老熟妇牲交

      <form id="9przj"></form>

          <form id="9przj"><th id="9przj"><th id="9przj"></th></th></form>

          <form id="9przj"></form>

          <noframes id="9przj"><form id="9przj"></form>